Yatayokusaidia Ikhlaasw katika kujifunza elimu

Swali: Ni njia zipi zinazomsaidia mtu juu ya kutafuta elimu?

Jibu: Miongoni mwa njia kubwa zinazomsaidia mtu juu ya Ikhlaasw ni mtu akusudie katika kujifunza elimu kutekeleza amri ya Allaah na kutarajia thawabu Zake. Kwa sababu Allaah amehimiza juu ya kujifunza elimu pale aliposema:

يَرْفَعِ اللَّـهُ الَّذِينَ آمَنُوا مِنكُمْ وَالَّذِينَ أُوتُوا الْعِلْمَ دَرَجَاتٍ

“Allaah atawainua wale walioamini miongoni mwenu na waliopewa elimu daraja za juu zaidi.”[1]

Atarajie kwa kufanya hivo yale aliyoahidi Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) pale aliposema:

“Yule ambaye Allaah anamtakia kheri basi humfahamisha dini.”

Vilevile anatakiwa kutambua kuwa hatokaa kikao chochote ambacho ndani yake anajifunza elimu isipokuwa kikao hichi kitakuwa ni ngawira kwake. Kwa msaada wa haya na mfano wake kutapatikana Ikhlaasw ndani ya moyo wake. Jengine ni kwamba mtu anapojifunza elimu basi akusudie uso wa Allaah na Pepo.

[1] 58:11

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (58) http://binothaimeen.net/content/1315
  • Imechapishwa: 01/07/2020