Swali: Kuna mtu alitawadha kwa ajili ya kuswali swalah ya dhuhaa kisha ukafika wakati wa Dhuhr. Je, inajuzu kwake kuswali Dhuhr kwa wudhu´ wa swalah ya Dhuhaa?
Jibu: Ndio. Akitawadha mtu kwa ajili ya kusoma Qur-aan au kuswali swalah ya dhuhaa bado anaendelea kubaki na wudhuu´ wake. Hivyo aswali Dhuhr, ´Aswr, Maghrib na ´Ishaa mpaka wudhuu´ wake uchenguke. Imethibiti ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) siku ya kufunguliwa mji wa Makkah aliswali swalah tano kwa wudhuu´ mmoja. Wakati ´Umar alipomuuliza na kusema: “Ee Mtume wa Allaah! Nimefanya jambo ambalo wewe hukufanya.” Akasema: “Ee ´Umar! Nilikusudia kufanya hivo.” Bi maana kwa ajili ya kubainisha kwamba inajuzu. Kwa hivyo mtu akitawadha kwa ajili ya kusoma Qur-aan, kuswali dhuhaa au akatawadha kwa ajili ya kuswali sunnah atakazoweza – hata kama itakuwa wakati usiokuwa wa dhuhaa – basi midhali yuko katika twahara aswali endapo utakuja wakati wa swalah.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (02) http://audio2.islamweb.net/lecturs/aalrrajhee/429/429.mp3
- Imechapishwa: 07/03/2018
Swali: Kuna mtu alitawadha kwa ajili ya kuswali swalah ya dhuhaa kisha ukafika wakati wa Dhuhr. Je, inajuzu kwake kuswali Dhuhr kwa wudhu´ wa swalah ya Dhuhaa?
Jibu: Ndio. Akitawadha mtu kwa ajili ya kusoma Qur-aan au kuswali swalah ya dhuhaa bado anaendelea kubaki na wudhuu´ wake. Hivyo aswali Dhuhr, ´Aswr, Maghrib na ´Ishaa mpaka wudhuu´ wake uchenguke. Imethibiti ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) siku ya kufunguliwa mji wa Makkah aliswali swalah tano kwa wudhuu´ mmoja. Wakati ´Umar alipomuuliza na kusema: “Ee Mtume wa Allaah! Nimefanya jambo ambalo wewe hukufanya.” Akasema: “Ee ´Umar! Nilikusudia kufanya hivo.” Bi maana kwa ajili ya kubainisha kwamba inajuzu. Kwa hivyo mtu akitawadha kwa ajili ya kusoma Qur-aan, kuswali dhuhaa au akatawadha kwa ajili ya kuswali sunnah atakazoweza – hata kama itakuwa wakati usiokuwa wa dhuhaa – basi midhali yuko katika twahara aswali endapo utakuja wakati wa swalah.
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (02) http://audio2.islamweb.net/lecturs/aalrrajhee/429/429.mp3
Imechapishwa: 07/03/2018
https://firqatunnajia.com/wudhuu-wa-swalah-ya-sunnah-kuuswalia-faradhi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)