Watu wengi hawajali ni aina ipi ya Ruqyah wanayotumia. Bali kila yule ambaye yasemekana kuwa anasomea watu na kuwatibu watu, wanaenda kwake. Bila kwanza kuhakikisha suala lake, wakajua ´Aqiydah yake na wakajua nini anachotumia katika Ruqyah; je, ni ya Kishari´ah au Shirki? Hawahakikisha mambo haya. Kinyume chake, wanachoamini wao ni umaarufu (wa msomaji) na utajo (wake kwa watu). Wanawatia khatarini ndugu na jamaa zao na Dini yao (kwa kwenda kwa watu kama hao). Suala hili ni khatari sana.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://youtu.be/ZW4t_k22f7E
  • Imechapishwa: 12/03/2018