1818- Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Nilimuomba Mola wangu wachanga ambapo akawanipa.” Nikamuuliza ni nini wachanga? Akasema: “Watoto wa watu.”

Ameipokea al-Mukhallas (09/23-24) kupitia Ahmad bin Yuusuf at-Taghlabiy ambaye amesema: Swafwaan bin Swaalih ametuhadithia: al-Waliyd ametuhadithia: ´Abdur-Rahmaan bin Hassaan al-Kitaaniy ametuhadithia: Muhammad bin al-Munkadir ametuhadithia, kutoka kwa Anas, kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

Tukikusanya njia zake zote naona kuwa Hadiyth ni nzuri na Allaah ndiye mjuzi zaidi.

Hadiyth hii ni dalili inayoonyesha kwamba watoto wa makafiri wataingia Peponi. Haya ndio maoni yenye nguvu, kama nilivyobainisha “Dhwilaal-ul-Jannah” (01/95).

  • Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Silsilat-ul-Ahaadiyth as-Swahiyhah (4/504)
  • Imechapishwa: 30/04/2019