Swali: Baada ya kumaliza kutawadha huhisi kuwa natokwa na matone ya mkojo. Je, ni lazima kwangu kurudi kutawadha kwa kuzingatia kwamba kila ninaporudia kutawadha nahisi hisia zilezile? Nifanye nini?
Jibu: Hisia hizi za muulizaji baada ya kutawadha huzingatiwa ni katika wasiwasi wa shaytwaan. Kwa hivyo si lazima kurudia kutawadha. Bali kilichowekwa katika Shari´ah kwake ni yeye kupuuzia jambo hilo na ahesabu kuwa wudhuu´ wake ni sahihi na haujachenguka. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema wakati alipoulizwa juu ya mtu ambaye anahisi kitu ndani ya swalah yake ambapo akasema:
“Asiondoke mpaka asikie sauti au ahisi harufu.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Isitoshe shaytwaan ni mwenye kupupia kuziharibu ´ibaadah za muislamu kukiwemo swalah, wudhuu´ na nyenginezo. Kwa hivyo ni lazima kumpiga vita na kutonyenyekea wasiwasi wake. Sambamba na hilo mtu amwombe Allaah ulinzi kutokamana na uchochezi na vitimbi vyake.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (10/124)
- Imechapishwa: 21/08/2021
Swali: Baada ya kumaliza kutawadha huhisi kuwa natokwa na matone ya mkojo. Je, ni lazima kwangu kurudi kutawadha kwa kuzingatia kwamba kila ninaporudia kutawadha nahisi hisia zilezile? Nifanye nini?
Jibu: Hisia hizi za muulizaji baada ya kutawadha huzingatiwa ni katika wasiwasi wa shaytwaan. Kwa hivyo si lazima kurudia kutawadha. Bali kilichowekwa katika Shari´ah kwake ni yeye kupuuzia jambo hilo na ahesabu kuwa wudhuu´ wake ni sahihi na haujachenguka. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema wakati alipoulizwa juu ya mtu ambaye anahisi kitu ndani ya swalah yake ambapo akasema:
“Asiondoke mpaka asikie sauti au ahisi harufu.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Isitoshe shaytwaan ni mwenye kupupia kuziharibu ´ibaadah za muislamu kukiwemo swalah, wudhuu´ na nyenginezo. Kwa hivyo ni lazima kumpiga vita na kutonyenyekea wasiwasi wake. Sambamba na hilo mtu amwombe Allaah ulinzi kutokamana na uchochezi na vitimbi vyake.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (10/124)
Imechapishwa: 21/08/2021
https://firqatunnajia.com/wasiwasi-wakati-wa-kutawadha/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)