Wasichana wa mke mtalikiwa ni Mahaarim wa yule mume wa pili?

Swali: Mwanamke mtalikiwa akiolewa na akazaa watoto wa kike kutoka kwa yule mume wa pili inafaa kwao kumsalimia [kwa kumbusu] usoni mume wa kwanza wa mama yao?

Jibu: Ndio, ni Mahaarim. Mwanamme akimuoa mwanamke na akamwingilia – ni lazima amwingilie –  akamwingilia au akamzalia wasichana kisha akamtaliki na akaolewa na mwanamme mwingine ambaye akamzalia watoto wa kike, watoto hao ni Mahaarim kwake. Watoto wa kambo. Inafaa kwao kumsalimia na inafaa kwake kuwasalimia. Bora salamu iwe shavuni, paji la uso, puani na mfano wake. Hivi ndio bora kuliko mdomoni.

Lakini akimuoa na akamtaliki pasi na kumwingilia. Kwa msemo mwingine amefunga naye ndoa peke yake na hakumwingilia, watoto wake wa kike watakuwa ni ajinabi kwake. Hawawi Mahaarim kwake; si kwa yule mume wa kabla yake wala mume wa baada yake.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/3803/هل-بنات-المطلقة-محارم-لزوجها-الاخر
  • Imechapishwa: 02/06/2022