Wanawake wanaofanya kupiga dufu harusini ndio kazi ya pato lao

Swali: Ni ipi hukumu ya kuajiri wanawake kuja kupiga dufu?

Jibu: Katika kazi za mkono si jambo zuri. Kupiga dufu katika mnasaba wa ndoa ni Sunnah kwa ajili ya kutangaza ndoa. Haitakikani mtu kufanya hii ndio kazi yake ya pato lake. Kutangaza Sunnah kunakusudiwa ndani yake mtu kupata ujira na hakukusudiwi tamaa ya kidunia.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/14775
  • Imechapishwa: 11/09/2020