Swali: Je, mwanafunzi anaweza kumhukumu mtu kuwa ni mtu wa Bid´ah au hili ni jambo maalum kwa wanachuoni tu?

Jibu: Kwanza ithibiti kweli kuwa jambo hili ni Bid´ah. Hakuna ajuaye hili isipokuwa wanachuoni. Hakuna ajuaye Bid´ah na Sunnah isipokuwa wanachuoni. Warejelewe wanachuoni na waulizwe kuhusu hili kama ni Bid´ah au sio Bid´ah.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (32) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/mo–1431-10-17.mp3
  • Imechapishwa: 15/11/2014