Wanachuoni wa leo kuhusu Qaadiyaaniyyah  

Kinacholengwa katika Hadiyth ni neno:

“Manabii wamekhitimishwa kwangu.” Muslim (523).

Hii ni dalili yenye kuonesha kuwa yeye ndiye Nabii wa mwisho na kwamba baada yake hakuna Mtume mwingine. Mwenye kuamini kuwa kuna Nabii mwingine atayekuja baada ya Muhammad ni kafiri na imani yake si sahihi. Kwa ajili hii mwenye kudai unabii baada yake ni kafiri kama mfano wa Musaylamah mwongo, Aswad al-´Ansiy na leo ni huyu Miyrzaa Ghulaam Ahmad al-Qaadiyaaniy ambaye amejitokeza leo na kudai kuwa ni Nabii. Qaadiyaaniyyah ni wale wanaomfuata huko India na wanaadhimisha mji wa Qaadiyaaniy na wanahiji katika mji huo. Hawa ni makafiri. Ni pote limetoka nje ya Uislamu na waislamu kama walivyothibitisha hilo wanachuoni. Wanachuoni wa leo wamekubaliana juu ya hilo.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajhiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Hidaayah ar-Rabbaaniyyah fiy Sharh al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah (01/132)
  • Imechapishwa: 31/05/2020