Wamemzika mtoto mchanga aliyezaliwa maiti nyumbani

Swali: Kuna mwanafunzi mmoja aniuliza hukumu ya kaburi la ndugu yao lilioko nyumbani mwao ambaye alizawali ameshakufa ambapo mama yao akamchimbia shimo refu kwenye kona moja ya nyumba na akamfukia. Sikuyajua hayo isipokuwa masiku machache yaliyopita na hivi sasa kumeshapita miaka nane. Ni ipi hukumu ya kumswalia nyumbani? Je, kaburi hili lkifukuliwe pamoja na kuzingatia kwamba huenda hata lisiwe na athari tena?

Jibu: Mosi ni wajibu kumswalia swalah ya jeneza.

Pili wanatakiwa kumfukua na kumzika makaburini. Nyumba sio mazikoni.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (54) http://binothaimeen.net/content/1227
  • Imechapishwa: 11/09/2019