Swali: Je, ´Umar al-Ashqar ni Salafiy?

Jibu: Kile ninachojua mimi ni kwamba ni Salafiy. Lakini sijui ni nini kilichompitikia siku za nyuma[1]. Ni kama mfano wa ´Abdur-Rahmaan ´Abdul-Khaaliq. Yeye ni Salafiy pia, lakini ametumbukia katika mambo ambayo si mazuri.

Swali: Kama mfano wa nini?

Jibu: Kama mfano uvyamauvyama, kuwafarikisha waislamu kwa jina la ukundiukundi. Anazipindisha Aayah na Hadiyth za kinabii. Katika kijitabu chake ”al-Muslimuun wal-´Amal as-Siyaasiy” anasema kuwa ni lazima kwa muislamu kufanya baadhi ya mambo ya haramu kwa ajili ya kutafuta kwake riziki yake. Maneno haya yako wapi na maneno Yake (Ta´ala):

وَمَن يَتَّقِ اللَّـهَ يَجْعَل لَّهُ مَخْرَجًا وَيَرْزُقْهُ مِنْ حَيْثُ لَا يَحْتَسِبُ

”Na yeyote anayemcha Allaah, basi atamjaalia njia ya kutokea na atamruzuku kutoka njia ambayo haitarajii.”[2]?

Aidha kuwapiga kwake vita Salafiyyuun ambao wana ´Aqiydah moja kama yake. Baadhi yao walikuwa ni wanafunzi wenzake katika chuo kikuu cha Kiislamu na mimi ndiye nilikuwa mwalimu wao. Kwa mfano Shaykh Muqbil myemeni.

[1] al-Albaaniy amesema 1417-04-09/1996-08-24:

”Shaykh ´Umar al-Ashqar alikuwa pamoja nasi ambaye baadaye alijiunga na al-Ikhwaan al-Muslimuun.” (Silsilat-ul-Hudaa wan-Nuur (930))

[2] 65:2-3

  • Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Silsilat-ul-Hudaa wan-Nuur (832)
  • Imechapishwa: 14/04/2020