Swali: Wako ambao wanafutu kwenye TV ya kwamba mayahudi na manaswara ni ndugu zetu katika imani. Ni ipi hukumu ya watu hawa? Wakufurishwe?

Jibu: Mwenye kusema kwamba mayahudi na manaswara ni ndugu zetu wanakufuru kwa hayo. Isipokuwa kama yule mwenye kusema hivo ni mjinga. Katika hali hiyo anatakiwa kuwekewa wazi. Akiendelea baada ya hapo ahukumiwe ukafiri. Akitubu Allaah anamsamehe.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Nawaaqidh-il-Islaam, uk. 96
  • Imechapishwa: 29/09/2018