Swali: Anayechinja kwa ajili ya kaburi amefanya Shirki. Je, aitwe Muislamu duniani na aitwe Muislamu na sio mshirikina?

Jibu: Vipi mshirikina aitwe Muislamu duniani!? Anayechinja kwa ajili ya asiyekuwa Allaah huyu ni mshirikina na sio Muislamu. Kuhusu kupewa udhuru. Kuhusu kupewa udhuru, yeye anaishi wapi? Anaishe angani au anaishi kati ya Waislamu na anasikia Qur-aan na maneno ya wanachuoni! Huyu sio mwenye kupewa udhuru. Lakini anawaiga waabudu makaburi na anatembea nao. Hataki kuuliza wala hataki kumsikiliza anayekataza hilo, anasema “Hawa ni Wahhaabiyyah wenye misimamo mikali”. Ujinga sio udhuru unaotumiwa kila siku. Una mipaka yake.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (27) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/mo–1431-5-11.mp3
  • Imechapishwa: 15/11/2014