Mambo ya ghaibu ambayo yanamtokea maiti katika kaburi lake na ni wajibu kuyaamini ni:

1 – Kuamini Munkar na Nakiyr

Akisema mwenye kusema: “Vipi wanamjia katika kaburi lake na sisi hatuwaoni?” Jibu tunasema kwamba Allaah ni Muweza juu ya kila jambo. Wewe kuna mambo mengi ambayo umefanywa huyaoni. Malaika hao wawili wanamjia na wewe huwaoni. Je, wewe unaona hewa inayoingia ndani ya mwili wako? Je, wewe unaona kila kitu? Kuna mambo mengi ambayo yapo na wewe huyaoni. Je, wewe unaiona akili yako? Si kila kitu usichokiona ni kwamba si sahihi. Haya ni maneno ya watu wanaoamini mazingira. Ama waumini wao wanaamini kila kilichothibiti katika khabari zake sahihi na wala hawayaingizi katika akili zao (na kuyapima kwanza).

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh al-Haaiyyah, uk. 164
  • Imechapishwa: 26/08/2020