2- ´Ubaadah bin as-Swaamit (Radhiya Allaahu ´anhu) alisema kumwambia mwanawe:
“Ee mwanangu! Hakika hutopata ladha ya imani mpaka kwanza ujue kuwa yaliyokufika hayakuwa yakukukosa na yaliyokukosa hayakuwa yakukufika. Nimemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema: “Kitu cha kwanza alichoumba Allaah ni kalamu. Akaiambia: “Andika.” Ikasema: “Ee Mola Wangu! Niandike nini?” Akasema: “Andika makadirio ya kila kitu mpaka kitaposimama Qiyaamah.” Ee mwanangu! Nimemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa salla) akisema: “Yule atakayekufa akiamini kinyume na hivi, basi huyo si katika mimi.”[1]
Mtoto wake anaitwa al-Waliyd bin ´Ubaadah bin as-Swaamit. Wakati ´Ubaadah alipokuwa anataka kukata roho ndipo mwanae akamuomba amuusie ambapo akamwambia amkaze na akasema:
“Ee mwanangu!”
Alisema hivo kwa sababu ya huruma na kumjali. Ni kama mfano wa Luqmaan aliposema:
يَا بُنَيَّ أَقِمِ الصَّلَاةَ وَأْمُرْ بِالْمَعْرُوفِ وَانْهَ عَنِ الْمُنكَرِ
“Ee mwanangu! Simamisha swalah na amrisha mema na kataza ya maovu.”[2]
Baba anatakiwa kuwausia wanae juu ya kumcha Allaah (´Azza wa Jall) na kushikamana na dini na ´Aqiydah. Huu ni wajibu wa kina baba juu ya watoto zao. Ni lazima kwao kuwausia kumcha Allaah, kuzitengeneza ´Aqiydah na kushikamana barabara na dini na tabia nzuri.
[1] Abu Daawuud (4700). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Dhwilaal-ul-Jannah” (111).
[2] 31:17
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: I´aanat-ul-Mustafiyd bi Sharh Kitaab-it-Tawhiyd, uk. 596
- Imechapishwa: 04/09/2019
2- ´Ubaadah bin as-Swaamit (Radhiya Allaahu ´anhu) alisema kumwambia mwanawe:
“Ee mwanangu! Hakika hutopata ladha ya imani mpaka kwanza ujue kuwa yaliyokufika hayakuwa yakukukosa na yaliyokukosa hayakuwa yakukufika. Nimemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema: “Kitu cha kwanza alichoumba Allaah ni kalamu. Akaiambia: “Andika.” Ikasema: “Ee Mola Wangu! Niandike nini?” Akasema: “Andika makadirio ya kila kitu mpaka kitaposimama Qiyaamah.” Ee mwanangu! Nimemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa salla) akisema: “Yule atakayekufa akiamini kinyume na hivi, basi huyo si katika mimi.”[1]
Mtoto wake anaitwa al-Waliyd bin ´Ubaadah bin as-Swaamit. Wakati ´Ubaadah alipokuwa anataka kukata roho ndipo mwanae akamuomba amuusie ambapo akamwambia amkaze na akasema:
“Ee mwanangu!”
Alisema hivo kwa sababu ya huruma na kumjali. Ni kama mfano wa Luqmaan aliposema:
يَا بُنَيَّ أَقِمِ الصَّلَاةَ وَأْمُرْ بِالْمَعْرُوفِ وَانْهَ عَنِ الْمُنكَرِ
“Ee mwanangu! Simamisha swalah na amrisha mema na kataza ya maovu.”[2]
Baba anatakiwa kuwausia wanae juu ya kumcha Allaah (´Azza wa Jall) na kushikamana na dini na ´Aqiydah. Huu ni wajibu wa kina baba juu ya watoto zao. Ni lazima kwao kuwausia kumcha Allaah, kuzitengeneza ´Aqiydah na kushikamana barabara na dini na tabia nzuri.
[1] Abu Daawuud (4700). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Dhwilaal-ul-Jannah” (111).
[2] 31:17
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: I´aanat-ul-Mustafiyd bi Sharh Kitaab-it-Tawhiyd, uk. 596
Imechapishwa: 04/09/2019
https://firqatunnajia.com/uwajibu-wa-baba-juu-ya-mwanae/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)