Swali: Mtu anayeishi katika mji amtii mtawala wa nchi anayotoka au mji aliyopo?

Jibu: Wakati mtu anaishi kwenye mji wa kikafiri kutoka na sababu sahihi, asitoke nje ya nidhamu za nchi. Ahakikishe anamtii Allaah na Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na asiende kinyume na nchi ile ili asende kinyume na sheria ya nchi kwa gharama ya mkono wake mwenyewe. Pasina kujali ni wapi Muislamu yuko anatakiwa kuwa ni kiigizo chema katika kheri na si shari.

  • Mhusika: ´Allaamah Swaalih bin Muhammad al-Luhaydaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Muhadhara: Haqiyqat-ul-Bay´ah fiyl-Islaam wa Bayaan Shuruwtihaa wa Khatwar Naz´ihaa
  • Imechapishwa: 05/09/2020