Suala hili kuhusu kuhukumu kinyume na aliyoteremsha Allaah ni katika mambo makubwa. Viongozi wengi wa leo wamepewa mtihani kwa jambo hilo. Hivyo basi, mtu asiwe na haraka ya kuwahukumu kwa kitu wasichostahiki mpaka pale watakapobainishiwa haki. Suala hili ni khatari. Tunamuomba Allaah (Ta´ala) azintengeneze hali za waislamu, watawala wao na nchi zao.

Vilevile ni wajibu kwa wale watu ambao Allaah amewapa elimu kuwabainishia watawala hawa haki ili wasiwe na udhuru wowote. Yule atayekufa, basi awe amekufa juu ya dalili, na yule atakayeishi, basi awe ameishi juu ya dalili. Mtu asijidogeshe na kumuogopa yeyote. Kwani hakika ya utukufu ni wa Allaah, Mtume Wake na waumini.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 159
  • Imechapishwa: 04/06/2020