Masuala ya mwanamke kuonyesha mapambo yake, kuonyesha uso wake, nyimbo na ufisadi mbalimbali ulioko Saudi Arabia. Kadhalika masuala ya Bid´ah na benki za ribaa zilizoko Saudi Arabia. Muislamu anadhani kuwa ni vizuri na ni Sunnah yakawepo Ufaransa, Marekani, Yemen au kwengineko [lakini si Saudi Arabia]. Sivyo hivyo. Ichukue dini yako kutoka katika Qur-aan na Sunnah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema, kama ilivyokuja katika “as-Swahiyh” ya Muslim:
“Hakika mimi nimekuachieni yale ambayo lau mtashikamana nayo barabara hamtopotea: Kitabu cha Allaah.”
Au Hadiyth yenye maana kama hiyo.
Chukua dini yako kutoka kwenye Qur-aan na Sunnah. Ama ufuataji kichwa mchunga unaofanywa hii leo unapelekea katika ufisadi. Huenda mtu wa kileo akadai kuwa ni katika Ahl-us-Sunnah ilihali TV iko nyumbani kwake. Mtu wa kileo akadai kuwa ni katika Ahl-us-Sunnah ilihali yuko na nyenzo ya kuchukua picha kando yake. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah amewalaani wenye kutengeneza picha.”
“Kila mtengeneza picha ni Motoni.”
“Hakika Malaika hawaingii nyumba ambayo ndani yake kuna mbwa wala picha.”
- Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ijaabatu as-Saa-il, uk. 334
- Imechapishwa: 29/09/2019
Masuala ya mwanamke kuonyesha mapambo yake, kuonyesha uso wake, nyimbo na ufisadi mbalimbali ulioko Saudi Arabia. Kadhalika masuala ya Bid´ah na benki za ribaa zilizoko Saudi Arabia. Muislamu anadhani kuwa ni vizuri na ni Sunnah yakawepo Ufaransa, Marekani, Yemen au kwengineko [lakini si Saudi Arabia]. Sivyo hivyo. Ichukue dini yako kutoka katika Qur-aan na Sunnah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema, kama ilivyokuja katika “as-Swahiyh” ya Muslim:
“Hakika mimi nimekuachieni yale ambayo lau mtashikamana nayo barabara hamtopotea: Kitabu cha Allaah.”
Au Hadiyth yenye maana kama hiyo.
Chukua dini yako kutoka kwenye Qur-aan na Sunnah. Ama ufuataji kichwa mchunga unaofanywa hii leo unapelekea katika ufisadi. Huenda mtu wa kileo akadai kuwa ni katika Ahl-us-Sunnah ilihali TV iko nyumbani kwake. Mtu wa kileo akadai kuwa ni katika Ahl-us-Sunnah ilihali yuko na nyenzo ya kuchukua picha kando yake. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah amewalaani wenye kutengeneza picha.”
“Kila mtengeneza picha ni Motoni.”
“Hakika Malaika hawaingii nyumba ambayo ndani yake kuna mbwa wala picha.”
Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ijaabatu as-Saa-il, uk. 334
Imechapishwa: 29/09/2019
https://firqatunnajia.com/usiwe-mwenye-kufuata-kichwa-mchunga/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)