Fawziy al-Bahrayniy amesema:

“Kuhusu mtazamo wa Rabiy´ al-Madkhaliy wa tamko “Jins-ul-´Amal”[1] ameliondosha katika imani pale anaposema:

“Tamko “Jins-ul-´Amal” halipatikani si katika Qur-aan wala Sunnah. Salaf hawakuzozana nalo na wala hawakuliingiza ndani ya imani.”

Tazama namna anavyoyaondosha matendo katika imani pale anaposema:

“… na wala hawakuliingiza ndani ya imani.”

Hii ni Irjaa´! Hii ni Irjaa´! Anayaondosha matendo katika imani ilihali Salaf waliyaingiza matendo katika imani na wakasema kuwa ni sehemu katika imani.”

1 – Naonelea kuwa asiyekuwa na matendo kabisa ni kafiri. Lakini mimi situmii tamko la “Jins-ul-´Amal” kwa sababu ya zile fitina linapelekea. Ninaliepuka kwa sababu ya kufunga njia za shari na uharibifu.

Ikiwa tamko “Jins-ul-´Amal” linapelekea katika Takfiyr basi nauliza Maswahabah na Taab´uun wanaangukia wapi, kwa sababu hawakusema yule asiyefanya tendo lolote jema ni kafiri. Kwa mujibu wa Haddaadiyyah ni Murji-ah.

Ikiwa kuzuia tamko “Jins-ul-´Amal” ina maana ya kuyaondosha matendo katika imani, yule ambaye hamkufurishi asiyeswali atakuwa ameiondosha swalah katika imani na kadhalika atakuwa yule asiyemkufurisha asiyeswali, asiyetoa zakaah, asiyefunga wala asiyeenda hajj ameyaondosha matendo haya makubwa katika imani. Wana haki zaidi ya kutuhumiwa Irjaa´. Kwa kuwa – kwa mujibu wa mfumo wa Haddaadiyyah – watakuwa wameyaondosha matendo haya makubwa katika imani. Tunajilinda kwa Allaah kutokana na mfumo wao na misingi yao ya batili inayosababisha shari, Tabdiy´ na mabalaa kwa Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah na maimamu wao wakubwa.

[1] Tazama https://firqatunnajia.com/neno-jins-ul-amal-limetoka-kwa-murji-ah/

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kashf Akaadhiyb wa Tahriyfaat wa Khiyaanaat Fawziy al-Bahrayniy, uk. 100
  • Imechapishwa: 09/10/2016