Ulazima wa thibitisha kwanza na kunasihiana

Laiti wanafunzi hii leo na vijana wangefuata mwenendo huu na wakathibitisha na wakaacha mambo haya ya migogoro na kuvutana kati yao. Kwa sababu ni ndugu na wanafunzi. ´Aqiydah yao ni moja. Wangeacha mizozo na tuhuma hizi na wakahakikisha juu ya yale yaliyoko baina yao. Kukithibiti kitu juu ya yale yaliyosemwa basi wanasihiane kati yao na wasilichukulie kulianika, kutuhumiana na kuzozana katika maneno. Kitendo hichi hakijuzu kabisa. Kilicho cha wajibu ni kuthibitisha kwanza. Kukithibiti basi anasihiwe yule ambaye kosa limethibiti kwake. Kwa sababu mtu hakukingwa na kukosea.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Aqiydatu al-Imaam-il-Mujaddid Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab, uk. 145
  • Imechapishwa: 26/01/2020