Swali: Baba na mama yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wako Peponi au Motoni?
Jibu: Baba na mama yake walikuwa katika kipindi cha kikafiri. Walikufa katika kipindi cha kikafiri. Imepokelewa katika Hadiyth:
“Hakika baba yangu na baba yako wako Motoni.”[1]
Alimuomba (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) Mola Wake amuombee msamaha hakupewa idhini. Kwa sababu alikufa katika kipindi cha kikafiri na juu ya dini ya watu wake ambayo ilikuwa ni kuabudu masanamu.
Swali: Je, mama yake si katika Ahl-ul-Fatrah?
Jibu: Udhahiri wa Hadiyth zinaonyesha kuwa ni miongoni mwa watu wa Motoni. Kwa sababu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliomba ruhusa amuombee msamaha lakini hakupewa ruhusa hiyo. Kuna uwezekano vilevile ikawa ni miongoni mwa Ahl-ul-Fatrah. Lakini imekuja katika baadhi ya mapokezi kwamba ni miongoni mwa watu wa Motoni kama mfano wa:
“Hakika baba yangu na baba yako wako Motoni.”
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake.
Swali: Je, walifikiwa na baadhi ya kitu katika mafunzo ya dini zilizotangulia?
Jibu: Pengine alifikiwa na khabari za dini ya Ibraahiym (´alayhis-Salaam), mambo ambayo yalifanya hoja kumsimamia.
Swali: Ibn Hishaam ametaja kwamba aliingia katika Uislamu. Unasemaje juu ya hilo?
Jibu: Hili halina msingi. Mwenye kusema kwamba baba na mama yake walisilimu ni khabari za batili.
[1] Muslim (203).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Kashf-ish-Shubuhaat, uk. 66-67
- Imechapishwa: 08/07/2019
Swali: Baba na mama yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wako Peponi au Motoni?
Jibu: Baba na mama yake walikuwa katika kipindi cha kikafiri. Walikufa katika kipindi cha kikafiri. Imepokelewa katika Hadiyth:
“Hakika baba yangu na baba yako wako Motoni.”[1]
Alimuomba (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) Mola Wake amuombee msamaha hakupewa idhini. Kwa sababu alikufa katika kipindi cha kikafiri na juu ya dini ya watu wake ambayo ilikuwa ni kuabudu masanamu.
Swali: Je, mama yake si katika Ahl-ul-Fatrah?
Jibu: Udhahiri wa Hadiyth zinaonyesha kuwa ni miongoni mwa watu wa Motoni. Kwa sababu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliomba ruhusa amuombee msamaha lakini hakupewa ruhusa hiyo. Kuna uwezekano vilevile ikawa ni miongoni mwa Ahl-ul-Fatrah. Lakini imekuja katika baadhi ya mapokezi kwamba ni miongoni mwa watu wa Motoni kama mfano wa:
“Hakika baba yangu na baba yako wako Motoni.”
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake.
Swali: Je, walifikiwa na baadhi ya kitu katika mafunzo ya dini zilizotangulia?
Jibu: Pengine alifikiwa na khabari za dini ya Ibraahiym (´alayhis-Salaam), mambo ambayo yalifanya hoja kumsimamia.
Swali: Ibn Hishaam ametaja kwamba aliingia katika Uislamu. Unasemaje juu ya hilo?
Jibu: Hili halina msingi. Mwenye kusema kwamba baba na mama yake walisilimu ni khabari za batili.
[1] Muslim (203).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Kashf-ish-Shubuhaat, uk. 66-67
Imechapishwa: 08/07/2019
https://firqatunnajia.com/ukweli-kuhusu-wazazi-wake-mtume-%d8%b5%d9%84%d9%89-%d8%a7%d9%84%d9%84%d9%87-%d8%b9%d9%84%d9%8a%d9%87-%d9%88%d8%b3%d9%84%d9%85/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)