Swali: Baadhi ya wale wenye hamasa wanatumia hoja kuwaua makafiri wenye ahadi [kwenye miji ya Waislamu] kwa sababu ndugu zetu Waislamu wanauawa ulimwenguni kote na wanasema kuwa watu hawa ni wapambanaji na hawana ahadi yoyote wala dhimma.

Jibu: Huyu kafiri mwenye ahadi ndiye ambaye amewaua ndugu zetu?

وَلَا تَزِرُ وَازِرَةٌ وِزْرَ أُخْرَىٰ

“Na wala mbebaji yeyoye [yule] hatobeba mzigo [wa dhambi wa mtu] mwengine.” (35:18)

Ukimuua yule ambaye amemuua Muislamu, pengine ukapewa nyudhuru fulani. Lakini unamuua mtu asiyekuwa na hatia:

وَلَا تَزِرُ وَازِرَةٌ وِزْرَ أُخْرَىٰ

“Na wala mbebaji yeyoye [yule] hatobeba mzigo [wa dhambi wa mtu] mwengine.”

Isitoshe jambo lingine ni kwamba ni haramu kuvunja ahadi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Yule anayemuua [kafiri] mwenye ahadi, hatonusa harufu ya Pepo.”

Haya ni matishio makali. Haijuzu kuvunja ahadi. Kumekuja matishio makali kuhusu hili. Hili linauchafua Uislamu na Waislamu.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Aqiydat-is-Saffaariniyyah (10) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/sfranih_10.mp3
  • Imechapishwa: 26/06/2018