Yahyaa al-Hajuuriy anasema lau Ahmad bin Hanbal atafufuka kutoka kwenye kaburi lake hatokubali maneno yake juu ya ´Abdur-Rahmaan [al-´Adniy]. Anasema pia kwamba lau wanachuoni wa dunia nzima watakubaliana juu ya kitu kingine kuliko kile anachosema juu ya [´Abdur-Rahmaan] al-´Adniy hatokubali hilo. Yuko tayari kuangusha maafikiano na kutojali.

Wakati nilipomwambia hilo Shaykh Rabiy´ akasema:

“Ni khatari zaidi kuliko Haddaadiyyah. Haddaadiyyah wanajificha nyuma ya wanachuoni na wanajionesha kuwa wanawapenda wakati huyu hajali kabisa wanachuoni.”

  • Mhusika: Shaykh ´Abdul-´Aziyz bin Yahyaa al-Bura´iy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.olamayemen.com/index.php?article_id=8861
  • Imechapishwa: 18/01/2017