Tayammum mtu anatakiwa kufanya kwa mpangilio na kwa kufuatanisha upesi

Swali: Katika Tayammum kumeshurutishwa kupangilia na kufuatanisha mbiombio?

Jibu: Ndio. Imeshurutishwa aanze kupangusa uso wake kisha vitanga vyake vya mikono. Hivyo ndivyo alivyofanya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipokuwa akimfunza ´Ammaar; alianza (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kupangusa uso wake kisha vitanga vyake vya mikono.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (6) http://alfawzan.af.org.sa/node/14379
  • Imechapishwa: 23/03/2017