Talaka ya sunnah inapita ila tu ikiwa mume kalazimishwa

Swali: Lini inapita Talaka ya Sunnah?

Jibu: Talaka ya Sunnah inapita moja kwa moja ikiwa kafanya hivyo kwa khiyari yake. Ama ikiwa mwenye kutaliki kalazimishwa, haipiti. Ama ikiwa kafanya hivyo kwa khiyari na ni mwenye akili anajua Talaka na hakulazimishwa, inapita kwa Ijmaa´. Ama Talaka ya Bid´ah, wanachuoni wametofautiana.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: www.alfawzan.af.org.sa/node/100000
  • Imechapishwa: 08/02/2018