Swali: Uwanja mahali kunaposwaliwa swalah ya ´iyd kunahesabika ni msikiti? Je, ni lazima kuswali Tahiyyat-ul-Masjid kabla ya kuanza kuswali swalah ya ´iyd au nyenginezo?

Jibu: Mahali kunaposwaliwa swalah ya ´iyd na mahali kunaposwali swalah ya kuomba mvua hakukuwi msikitini muda wa kuwa hakuswaliwi vile vipindi vya swalah tano. Msikiti ni ile sehemu ambayo kunaswaliwa zile swalah tano. Ama uwanja wa kuswalia ´iyd na swalah ya kuomba mvua hakuswaliwi  Tahiyyat-ul-Masjid.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (11) https://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=FullContent&audioid=191491#219817
  • Imechapishwa: 28/05/2019