Swali: Watu wanayarudirudi maneno:

“Fungeni mtapata afya njema.”

Jibu: Kumepokelewa Hadiyth juu ya hilo lakini si Swahiyh. Haikuthibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hata hivyo hapana shaka kwamba swawm inaipa afya njema mwili kutokana na yale matendo mema yaliyo ndani yake, mwili kuepuka mchanganyiko wa vyakula na kuuzowesha mwili subira. Ni sahihi kwamba ndani yake kun kuwa na sifa njema.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://www.youtube.com/watch?v=bh2DpsHpwcU
  • Imechapishwa: 10/05/2020