Swali: Baadhi ya watu wanaswali Tarawiyh nyuma ya imamu. Lakini imamu anaposimama kuswali Witr wanajitenga na imamu.
Jibu: Huku ni kwenda kinyume na Sunnah. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yule atakayesimama pamoja na imamu mpaka akamaliza, basi anaandikiwa usiku mzima.”
Yule anayetaka kupata thawabu kamilifu kutoka kwa Allaah (´Azza wa Jall) asijitenge na imamu.
Kama anataka kuendelea kusimama mwishoni mwa usiku afanye hivo hata kama ni baada ya kuswali Witr pamoja na imamu. Asimame tena nyumbani kwake na wala asikariri Witr kwa mara nyingine. Ile Witr aliyoswali pamoja na imamu inamtosha. Baadhi ya watu wanajitenga na imamu kwa hoja eti wataswali mwishoni mwa usiku na kwamba wanachelewesha Witr mpaka mwishoni mwa usiku. Huku ni kwenda kinyume na kilicho bora zaidi. Bora ni yeye kusimama pamoja na imamu mpaka amalize kuswali Witr pamoja na imamu. Akisimama mwishoni mwa usiku hahitajii kuswali Witr nyingine.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://www.youtube.com/watch?v=2vQdgZLzLuI
- Imechapishwa: 11/05/2020
Swali: Baadhi ya watu wanaswali Tarawiyh nyuma ya imamu. Lakini imamu anaposimama kuswali Witr wanajitenga na imamu.
Jibu: Huku ni kwenda kinyume na Sunnah. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yule atakayesimama pamoja na imamu mpaka akamaliza, basi anaandikiwa usiku mzima.”
Yule anayetaka kupata thawabu kamilifu kutoka kwa Allaah (´Azza wa Jall) asijitenge na imamu.
Kama anataka kuendelea kusimama mwishoni mwa usiku afanye hivo hata kama ni baada ya kuswali Witr pamoja na imamu. Asimame tena nyumbani kwake na wala asikariri Witr kwa mara nyingine. Ile Witr aliyoswali pamoja na imamu inamtosha. Baadhi ya watu wanajitenga na imamu kwa hoja eti wataswali mwishoni mwa usiku na kwamba wanachelewesha Witr mpaka mwishoni mwa usiku. Huku ni kwenda kinyume na kilicho bora zaidi. Bora ni yeye kusimama pamoja na imamu mpaka amalize kuswali Witr pamoja na imamu. Akisimama mwishoni mwa usiku hahitajii kuswali Witr nyingine.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://www.youtube.com/watch?v=2vQdgZLzLuI
Imechapishwa: 11/05/2020
https://firqatunnajia.com/swali-tarawiyh-nyuma-ya-imamu-hadi-mwisho/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)