Suurah zinazosomwa katika swalah ya ´Iyd

Swali: Ni Suurah zipi ambazo imependekezwa kwa imamu kuzisoma katika swalah ya ´Iyd baada ya kusoma al-Faatihah?

Jibu: Imependekezwa kusoma ima Suurah “Qaaf” na “Iqtarab” au Suurah “al-A´laa” na “al-Ghaashiyah”. Hii ndio Sunnah. Akisoma zengine pia ni sawa.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawa (16/245)
  • Imechapishwa: 14/06/2018