Sujuud-ut-Tilaawah kwa kuashiria

Swali: Mtu anaweza kufanya Sujuud-ut-Tilaawah kwa kuashiria?

Jibu: Ndio, ikiwa hawezi kusujudu katika ardhi. Ijulikane kuwa Sujuud-ut-Tilaawah imependekezwa, sio faradhi. Ikiwa hawezi kusujudu katika ardhi asujudu kwa kuinama. Katika hali hiyo atakuwa ameipata Sunnah. Hata hivyo atakuwa si mwenye kuipata Sunnah wala fadhila yoyote ikiwa anaweza kusujudu katika ardhi na asifanye hivo.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (01) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/omdh–14340126_0.mp3
  • Imechapishwa: 25/08/2020