Swali: Ni miongoni mwa wale watu ambao wanawaficha watu ukhalifu wao na wala simfichi Allaah, wale wanaowaamrisha watu mema ilihali wao wenyewe hawayafanyi, wanakataza maovu ilihali wao wenyewe wanayafanya, sisimami usiku kuswali na wala sisomi Qur-aan. Nina miaka ishirini na sita. Sijawahi kukhitimisha Qur-aan isipokuwa takriban mara tano tu. Nataraji kutoka kwa Allaah kisha kwako uniawaidhi na unipe nasaha. Huenda Allaah akaninufaisha mimi na wale waliohudhuria kwazo.

Jibu: Hapana shaka kwamba sote ni wenye mapungufu. Lakini mambo haya ni baina yako wewe na Allaah. Tubu kwa Allaah baina yako wewe na Allaah. Usiwatajie mambo haya watu. Mambo haya ni baina yako wewe na Allaah. Tubu kwa Allaah, pupia kumtii Allaah na Allaah atakusaidia.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Nawaaqidh-il-Islaam (09) http://ajurry.com/safrawy/chorohat-elakida/chorohat-nawakid-elislam/charh-salah-fawzan/09.mp3
  • Imechapishwa: 30/03/2019