al-Halabiy amesema:

“Tofauti inaweza kuhusiana na kwamba – pamoja na kuwa tuna makosa ya Abul-Hasan al-Maghraawiy na tulifuatilia baadhi ya makosa hayo pamoja na wao – hatuwatoi katika Salafiyyah. Hili ni suala lingine.”

Hapa Shaykh ´Aliy al-Halabiy anakubali mwenyewe kuwa alichukulia usahali kwa al-Ma´ribiy na al-Maghraawiy na makemeo yake hayakuwa ya kweli. Kwa vile amesema:

“… na tulifuatilia baadhi ya makosa hayo pamoja na wao…”

Kuna uwezekano mkubwa mapambano haya hayakuwa ya kikweli. Simkadhibishi Shaykh, lakini mapambano ni lazima yawe yamepigwa bila ya hisia na hasira. Hasira zetu kwa ajili ya Allaah zinatakiwa kuwa kali na pale tunapokemea yale Anayochukia, tunayakemea kwa ukali.

  • Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: ad-Durar an-Najmiyyah fiy Radd-ish-Shubuhaat al-´Aqadiyyah wal-Manhajiyyah, uk. 378-379
  • Imechapishwa: 18/03/2017