Sio lazima kumtaliki mke wakati wa kuongeza mwingine

Swali: Nimeoa mke wa pili, lakini mke wa kwanza ananiomba Talaka kwa hoja ya kwamba anakhofia juu ya Dini yake kutokana na wingi wa wivu. Je, nimpe Talaka?

Jibu: Sio lazima. Ni juu yako kuwa muadilifu na wala sio lazima. Ni juu yako kumkinaisha na umlinganie katika usawa na uongee naye kwa upole na kwa maneno mazuri mpaka uweze kumkinaisha na wala usiharakishe kutoa Talaka. Pengine Allaah Akamtuliza. Ni lazima kwako kufanya uadilifu.

  • Mhusika: Imaaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://subulsalam.com/play.php?catsmktba=12796
  • Imechapishwa: 20/11/2014