“Sikubali unioe mpaka umuoe pia rafiki yangu”

Swali: Wakati mwanaume alipomposa mwanamke, aliweka sharti ya kwamba anatakiwa vilevile kumuoa rafiki yake. Unaonaje kuhusu sharti hii?

an-Najmiy: Nini? Kumuoa nani?

Muulizaji: Rafiki yake.

Jibu: Mwanaume amuoe? Ikiwa watakubaliana hivyo itakuwa inajuzu. Mlango uko wazi mbele yake. Ikiwa wanawake wote wawili watakubaliana hilo hakuna kizuizi. Tuwaambie nini? Kwamba haijuzu? Hapana.

  • Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.sahab.net/forums/showthread.php?t=351323
  • Imechapishwa: 20/09/2020