Swali: Je, inajuzu kula vichinjwa vya Ahl-ul-Kitaab pasi na sharti zozote?

Jibu: Sharti iwe wamechinja kwa njia ya Kishari´ah. Ama ikiwa wanachinja kinyume na njia ya Kishari´ah, kama kwa kutumia umeme, haijuzu sawa ikiwa kwa Waislamu wala Ahl-ul-Kitaab. Ni lazima kuchinja iwe kwa njia ya Kishari´ah.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/eg–14340421.mp3
  • Imechapishwa: 20/09/2020