Swali: Kuna mtu ana ugonjwa wa moyo na haiwezi kufanya kazi vizuri isipokuwa mpaka atumie dawa kwa muendelezo kila baada ya saa nane au sita. Je, swawm yake inaanguka?

Jibu: Ndio, swawm yake inaanguka na badala yake anatakiwa kulisha kwa kila siku moja masikini. Akitaka anaweza kumpa kila masikini robo pishi ya mchele. Akimpa pia na nyama ndio bora zaidi. Akitaka vilevile anaweza kuwaalika chakula cha jioni au cha mchana ule usiku wa mwisho wa Ramadhaan. Yote hayo yanajuzu.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (19/126)
  • Imechapishwa: 19/06/2017