Swali: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atakayefunga Ramadhaan kwa imani na matarajio, basi atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia.”
Je, madhambi haya kunaingia pia madhambi makubwa?
Jibu: Hapa wanachuoni wametofautiana. Maoni sahihi ni kwamba hayahusiana na madhambi makubwa. Ni lazima mtu atubie juu ya madhambi makubwa. Inahusiana na madhambi madogo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Swalah tano, ijumaa mpaka ijumaa nyingine, Ramadhaan mpaka Ramadhaan nyingine vinafuta yale yaliyo baina yake midhali mtu atajiepusha madhambi makubwa.”
Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
إِن تَجْتَنِبُوا كَبَائِرَ مَا تُنْهَوْنَ عَنْهُ نُكَفِّرْ عَنكُمْ سَيِّئَاتِكُمْ
“Mkijiepusha na madhambi makubwa mnayokatazwa, basi Tutakufutieni madhambi yenu madogo.” (04:31)
Kilicho wazi katika dalili ni kwamba kusamehewa kunakuwa katika madhambi madogo. Madhambi madogo ndio ambayo yanafutwa kwa kutenda matendo mema. Kuhusu madhambi makubwa ni lazima mtu atubie.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaam al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/14891
- Imechapishwa: 06/06/2017
Swali: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atakayefunga Ramadhaan kwa imani na matarajio, basi atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia.”
Je, madhambi haya kunaingia pia madhambi makubwa?
Jibu: Hapa wanachuoni wametofautiana. Maoni sahihi ni kwamba hayahusiana na madhambi makubwa. Ni lazima mtu atubie juu ya madhambi makubwa. Inahusiana na madhambi madogo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Swalah tano, ijumaa mpaka ijumaa nyingine, Ramadhaan mpaka Ramadhaan nyingine vinafuta yale yaliyo baina yake midhali mtu atajiepusha madhambi makubwa.”
Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
إِن تَجْتَنِبُوا كَبَائِرَ مَا تُنْهَوْنَ عَنْهُ نُكَفِّرْ عَنكُمْ سَيِّئَاتِكُمْ
“Mkijiepusha na madhambi makubwa mnayokatazwa, basi Tutakufutieni madhambi yenu madogo.” (04:31)
Kilicho wazi katika dalili ni kwamba kusamehewa kunakuwa katika madhambi madogo. Madhambi madogo ndio ambayo yanafutwa kwa kutenda matendo mema. Kuhusu madhambi makubwa ni lazima mtu atubie.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaam al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/14891
Imechapishwa: 06/06/2017
https://firqatunnajia.com/ramadhaan-inafuta-madhambi-makubwa-ya-mtu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)