Swali: Kwa kutegemea Hadiyth ya Bilaal (Radhiya Allaahu ´anh):
“Sikupatapo kutawadha isipokuwa niliswali Rak´ah mbili baada ya wudhuu´.”
Mimi baadhi ya nyakati natawadha wakati uliokatazwa kuswali ndani yake. Mfano wa hilo ni baada ya swalah ya ´Aswr, baada ya swalah ya Fajr au wakati wa kuzama kwa jua na wakati wa kuchomoza kwake. Je, ninapata dhambi nikiswali Rak´ah mbili za wudhuu´?
Jibu: Kilichopendekezwa ni wudhuu´. Kilichopendekezwa ni mtu kutawadha na kuswali Rak´ah mbili ambazo ni Sunnah ya wudhuu´ katika wakati wowote hata kama ni wakati uliokatazwa. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kutawadha mfano wa wudhuu´ wangu huu kisha akaswali Rak´ah mbili na asiizungumzishe nafsi yake kati ya mawili hayo, basi Allaah atamsamehe dhambi zake zilizotangulia.”
Kinacholengwa ni kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akitawadha basi anaswali Rak´ah mbili na akawakokoteza watu kufanya hivo. Zinaitwa “Sunnat-ul-Wudhuu´”. Hakuna neno kuziswali wakati uliokatazwa na wakati mwingineo. Kwa sababu ni Sunnah iliyokokotezwa.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/9505/%D8%AD%D9%83%D9%85-%D8%B1%D9%83%D8%B9%D8%AA%D9%8A-%D8%A7%D9%84%D9%88%D8%B6%D9%88%D8%A1-%D9%88%D8%B5%D9%84%D8%A7%D8%AA%D9%87%D8%A7-%D9%81%D9%8A-%D8%A7%D9%88%D9%82%D8%A7%D8%AA-%D8%A7%D9%84%D9%86%D9%87%D9%8A
- Imechapishwa: 21/02/2020
Swali: Kwa kutegemea Hadiyth ya Bilaal (Radhiya Allaahu ´anh):
“Sikupatapo kutawadha isipokuwa niliswali Rak´ah mbili baada ya wudhuu´.”
Mimi baadhi ya nyakati natawadha wakati uliokatazwa kuswali ndani yake. Mfano wa hilo ni baada ya swalah ya ´Aswr, baada ya swalah ya Fajr au wakati wa kuzama kwa jua na wakati wa kuchomoza kwake. Je, ninapata dhambi nikiswali Rak´ah mbili za wudhuu´?
Jibu: Kilichopendekezwa ni wudhuu´. Kilichopendekezwa ni mtu kutawadha na kuswali Rak´ah mbili ambazo ni Sunnah ya wudhuu´ katika wakati wowote hata kama ni wakati uliokatazwa. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kutawadha mfano wa wudhuu´ wangu huu kisha akaswali Rak´ah mbili na asiizungumzishe nafsi yake kati ya mawili hayo, basi Allaah atamsamehe dhambi zake zilizotangulia.”
Kinacholengwa ni kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akitawadha basi anaswali Rak´ah mbili na akawakokoteza watu kufanya hivo. Zinaitwa “Sunnat-ul-Wudhuu´”. Hakuna neno kuziswali wakati uliokatazwa na wakati mwingineo. Kwa sababu ni Sunnah iliyokokotezwa.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/9505/%D8%AD%D9%83%D9%85-%D8%B1%D9%83%D8%B9%D8%AA%D9%8A-%D8%A7%D9%84%D9%88%D8%B6%D9%88%D8%A1-%D9%88%D8%B5%D9%84%D8%A7%D8%AA%D9%87%D8%A7-%D9%81%D9%8A-%D8%A7%D9%88%D9%82%D8%A7%D8%AA-%D8%A7%D9%84%D9%86%D9%87%D9%8A
Imechapishwa: 21/02/2020
https://firqatunnajia.com/rakah-mbili-za-wudhuu-kuziswali-wakati-uliyokatazwa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)