al-Halabiy amesema:

“Tofauti inaweza kuhusiana na kwamba – pamoja na kuwa tuna makosa ya Abul-Hasan al-Maghraawiy na tulifuatilia baadhi ya makosa hayo pamoja na wao – hatuwatoi katika Salafiyyah. Hili ni suala lingine.”

Ni kwa nini hamkuwatoa katika Salafiyyah wakati Bid´ah ziko wazi kabisa na kubwa? Kusoma kipeperushi kuhusu al-Maghraawiy kutoka kwenye mkanda wake na kutabainika wazi wazi ya kuwa ni Khaarijiy aliyeungua. Kuhusiana na al-Ma´ribiy, ana Bid´ah nyenginezo. Vilevile niu swahiba wa al-Maghraawiy. Je, jambo hili lina utatizi kiasi cha kwamba mnasita kuwatoa katika Salafiyyah?

Vinginevyo ni zipi fikira za Khawaarij? Je, sio kuwakufurisha waislamu? Sio kuhalalisha damu zao, mali zao na heshima zao? Hawakuhalalisha damu ya ´Uthmaan (Radhiya Allaahu ´anh)? Hawakuhalalisha damu ya ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh)? Hawakuhalalisha damu ya ´Abdullaah bin Khabbaab (Radhiya Allaahu ´anh)? Hawakulipasua tumbo la mwanamke wake? al-Muhallab bin Abiy Swufrah hakuteua kuwapiga vita Khawaarij katika zama za Banuu Umayyah? Je, Khawaarij hawakufanya uasi mara kwa mara katika zama za Banuul-´Abbaas? Je, hawakuhalalisha damu ya viumbe bora kabisa katika kila zama? Hivi kweli hamuoni uchupaji wote huu, Takfiyr na milipuko inayoendelea hivi sasa? Soma vitabu vilivyoandika mapokezi ya Salaf. Je, mnaweza kumpata yeyote katika Salaf ambaye amewaingiza Khawaarij katika mfumo Salaf na Salafiyyuun? Au kinyume chake waliwakaripia, wakawakemea na kuwazingatia ni katika aina mbaya zaidi ya watu wa Bid´ah?

  • Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: ad-Durar an-Najmiyyah fiy Radd-ish-Shubuhaat al-´Aqadiyyah wal-Manhajiyyah, uk. 379-380
  • Imechapishwa: 18/03/2017