Swali: Imethibiti katika Hadiyth ya kwamba Allaah Hushuka katika mbingu mwishoni mwa theluthi ya usiku na Hunadi kwa wanaoomba maghfirah. Je, katika Hadiyth hii kuna dalili na Radd kwa mwenye kusema ya kwamba Allaah hazungumzi?

Jibu: Ndio, kuna Radd ya wazi. Husema “Ni nani anayeniomba nimpe? Ni nani anayeniomba msamaha nimsamehe? Kuna anayetubia nimsamehe? Kuna anayeniuliza nimpe? Kuna wanaoniomba msamaha niwasamehe?” Haya ni maneno ya Allaah (Jalla wa ´Alaa).

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (63) http://www.alfawzan.af.org.sa/node/13810
  • Imechapishwa: 16/11/2014