Rabiy´ al-Madkhaliy anaipenda Sunnah na Ahl-us-Sunnah

Swali: Shaykh Rabiy´ (Hafidhwahu Allaah) amezidi kutukanwa sana. Tunataraji kutoka kwako kama unaweza kusema ukweli kuhusu Shaykh huyu mtukufu ili kumwangazia yule anayetafuta haki.

Jibu: Shaykh Rabiy´ namjua kutoka katika mji wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ni Shaykh na Sunniy. Anaipenda Sunnah ya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na Ahl-us-Sunnah. Pamoja na hivyo ni mwanaadamu ambaye anapatia na anakosea, kuna anayoyajua na kuna asiyoyajua. Sisi pia ni vivyo hivyo, mara tunajua na mara hatujui.

Himdi zote zinamstahikia Allaah amebainisha upotevu wa watu wengi wa hii leo. Ilikuwa ni kipindi ambacho hakuna mwengine zaidi ya Shaykh al-Albaaniy na mimi tu ndio tunawakemea Hizbiyyuun. Pindi ndugu Rabiy´ alipoandika vitabu vyake barabara, ndipo yakapitika yale tuliokuwa tukiyatarajia na yale yaliyowasibu wengine. Watu wa Bid´ah wanawahujumu Ahl-us-Sunnah tangu hapo kale.

  • Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://muqbel.net/sounds.php?sound_id=15
  • Imechapishwa: 09/04/2017