Raafidhwah wanawasaidia makafiri dhidi ya waislamu

Hii ndio hali ya Ahl-ul-Bid´ah wanaokwenda kinyume na Qur-aan na Sunnah. Hakuna kingine wanachofuata isipokuwa tu dhana na yale wanayotamani nafsi zao. Wako na ujinga na dhuluma na khaswakhaswa Raafidhwah. Wako na matamanio makubwa kutokana na ujinga na dhuluma. Wako na chuki kubwa kabisa juu ya mawalii wa Allaah baada ya Mitume miongoni mwa wale watu wa mwanzo kati ya Muhaajiruun na Answaar na wale wenye kuwafuata kwa wema – Allaah amewaridhia na wao wamemridhia.

Sambamba na hilo wanawapenda makafiri na wanafiki katika mayahudi, manaswara, washirikina na wakanamungu kama vile Nusayriyyah, Ismaa´iyliyyah na wengineo katika wapotevu. Utawaona, au wengi wao, wanasimama upande wa makafiri dhidi ya waislamu pasi na kujali tofauti ni ya kimaneno au ya matendo, kama vile vita. Hiki ni kitu watu wana uzowefu nacho mara nyingi. Kwa mfano Raafidhwah waliwasaidia washirikina wa kituruki na wengineo dhidi ya waislamu wa Khurasaan, ´Iraaq, Jaziyrah, Shaam na sehemu nyenginezo. Kama tulivyosema hayo yamekwishatokea mara nyingi. Katika vita vikubwa na vibaya sana ni vile vilivyotokea miaka ya 400 na 700. Wakati ambapo makafiri wa kituruki walipofika katika mji wa waislamu na wakaua idadi kubwa ya waislamu ambayo hakuna anayeitambua isipokuwa Allaah pekee. Raafidhwah walikuwa ni watu wenye chuki zaidi dhidi ya waislamu na wakawapa msaada mkubwa makafiri. Kadhalika ushirikiano wao mkubwa na mayahudi unatambulika, mpaka watu wakawa wanawaita “punda wa mayahudi”.

  • Mhusika: Shaykh-ul-Islam Ahmad bin Taymiyyah
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Minhaaj-us-Sunnah an-Nabawiyyah (1/20-21)
  • Imechapishwa: 03/02/2019