Qudaamah bin Madh´uun alikuwa ni Abu ´Amr al-Jumhiy. Ni miongoni mwa wale waislamu waliotangulia mwanzo ambao wameshirika vita vya Badr. Alikuwa ni kiongozi wa Bahrayn wakati wa ´Umar. Alikuwa ni mjomba wake mama wa waumini Hafswah na Ibn ´Umar. Alikuwa amemuoa shangazi yao Hafswah bint al-Khattwaab, mmoja katika wanawake waliofanya Hijrah.
Qudaamah alifanya Hijrah kwenda Uhabeshi. Kuna kipindi alikunywa pombe kutokana na kuelewa kimakosa maneno ya Allaah (Ta´ala):
لَيْسَ عَلَى الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ جُنَاحٌ فِيمَا طَعِمُوا
“Hakuna dhambi juu ya wale walioamini na wakatenda mema katika vile walivyokula [kabla ya kuharimishwa]… “[1]
´Umar akampiga bakora na akamwondoa kutoka Bahrayn.
Ayyuub as-Sikhtiyaaniy amesema:
“Mtu pekee aliyeshiriki vita vya Badr na akapigwa bakora ni yeye.”
Sivyo hivo. Kuna mwingine tena: Nu´aymaan bin ´Amr al-Answaariy an-Najjaariy mfanya mzaha.
Ibn Sa´d amesema:
“Watoto wa Qudaamah alikuwa ´Umar, Faatwimah na ´Âishah. Alifanya Hijrah ya pili kwenda Uhabeshi na alishuhudia vita vya Badr na Uhud.”
´Aaishah bint Qudaamah amesema kuwa baba yake alikufa mwaka wa 36. Aliishi miaka 68. Alikuwa hazipaki rangi mvi zake. Alikuwa mrefu na kahawia. Allaah amuwie radhi.
[1] 5:93
- Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (1/161-162)
- Imechapishwa: 18/01/2021
Qudaamah bin Madh´uun alikuwa ni Abu ´Amr al-Jumhiy. Ni miongoni mwa wale waislamu waliotangulia mwanzo ambao wameshirika vita vya Badr. Alikuwa ni kiongozi wa Bahrayn wakati wa ´Umar. Alikuwa ni mjomba wake mama wa waumini Hafswah na Ibn ´Umar. Alikuwa amemuoa shangazi yao Hafswah bint al-Khattwaab, mmoja katika wanawake waliofanya Hijrah.
Qudaamah alifanya Hijrah kwenda Uhabeshi. Kuna kipindi alikunywa pombe kutokana na kuelewa kimakosa maneno ya Allaah (Ta´ala):
لَيْسَ عَلَى الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ جُنَاحٌ فِيمَا طَعِمُوا
“Hakuna dhambi juu ya wale walioamini na wakatenda mema katika vile walivyokula [kabla ya kuharimishwa]… “[1]
´Umar akampiga bakora na akamwondoa kutoka Bahrayn.
Ayyuub as-Sikhtiyaaniy amesema:
“Mtu pekee aliyeshiriki vita vya Badr na akapigwa bakora ni yeye.”
Sivyo hivo. Kuna mwingine tena: Nu´aymaan bin ´Amr al-Answaariy an-Najjaariy mfanya mzaha.
Ibn Sa´d amesema:
“Watoto wa Qudaamah alikuwa ´Umar, Faatwimah na ´Âishah. Alifanya Hijrah ya pili kwenda Uhabeshi na alishuhudia vita vya Badr na Uhud.”
´Aaishah bint Qudaamah amesema kuwa baba yake alikufa mwaka wa 36. Aliishi miaka 68. Alikuwa hazipaki rangi mvi zake. Alikuwa mrefu na kahawia. Allaah amuwie radhi.
[1] 5:93
Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (1/161-162)
Imechapishwa: 18/01/2021
https://firqatunnajia.com/qudaamah-bin-madhuun-radhiya-allaahu-anh/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)