Swali: Je, inafaa kwa mwanamke kumpa zawadi ya sanduku la manukato mwanamke mwingine pamoja na kuzingatia kwamba mwanamke anayepewa zawadi hutoka kwenda mtaani hali ya kuwa amejitia manukato haya? Je, mtoa zawadi pia anapata dhambi?
Jibu: Hakuna neno kumpa manukato mwanamke. Kwa sababu zawadi inaleta mapenzi na mahaba. Mtoa zawadi anapata thawabu. Mwanamke huyu aliyepewa zawadi akiyatumia manukato haya kwa njia haramu basi dhambi anapata yeye. Lakini ikiwa mtoa zawadi huyu anajua kuwa mwanamke huyu anayetaka kumpa zawadi atayatumia manukato haya katika kutoka kwenda sokoni basi haijuzu kwake kumpa. Kwa sababu hiyo ina maana ya kumsaidia katika dhambi na uadui. Amesema (Ta´ala):
وَلَا تَعَاوَنُوا عَلَى الْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ
“… na wala msisaidiane katika dhambi na uadui.”[1]
[1] 05:02
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (10/42)
- Imechapishwa: 06/08/2021
Swali: Je, inafaa kwa mwanamke kumpa zawadi ya sanduku la manukato mwanamke mwingine pamoja na kuzingatia kwamba mwanamke anayepewa zawadi hutoka kwenda mtaani hali ya kuwa amejitia manukato haya? Je, mtoa zawadi pia anapata dhambi?
Jibu: Hakuna neno kumpa manukato mwanamke. Kwa sababu zawadi inaleta mapenzi na mahaba. Mtoa zawadi anapata thawabu. Mwanamke huyu aliyepewa zawadi akiyatumia manukato haya kwa njia haramu basi dhambi anapata yeye. Lakini ikiwa mtoa zawadi huyu anajua kuwa mwanamke huyu anayetaka kumpa zawadi atayatumia manukato haya katika kutoka kwenda sokoni basi haijuzu kwake kumpa. Kwa sababu hiyo ina maana ya kumsaidia katika dhambi na uadui. Amesema (Ta´ala):
وَلَا تَعَاوَنُوا عَلَى الْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ
“… na wala msisaidiane katika dhambi na uadui.”[1]
[1] 05:02
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (10/42)
Imechapishwa: 06/08/2021
https://firqatunnajia.com/pindi-utapojua-kuwa-mwanamke-atatumia-manukato-wakati-anapotoka-nje/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)