Swali: Ni ipi hukumu ya kumchukua picha mtu na khaswa upande wa uso wake?

Jibu: Kukiondoshwa kichwa kutoka kichwani yanaondoka makatazo. Picha isiyokuwa na kichwa haina neno. Kwa msemo mwingine ni kwamba kichwa chote kinatakiwa kuondoshwa na sio uso peke yake. Pindi kichwa kinaondoshwa basi yanapotea makatazo. Kichwa kikikatwa na kuondoshwa basi yameondoka makatazo. Haitoshi kuweka msitari; ni lazima kuondosha kichwa. Kichwa chote kinapaswa kuondoshwa ili uso ubaki bila kichwa. Makatazo yanaondoka na hivyo Malaika wanaweza kuingia ndani. Lakini muda wa kuwa bado kichwa kipo basi hayo ndio yamekatazwa.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://www.youtube.com/watch?v=4xTg13fHGuU
  • Imechapishwa: 13/09/2020