Swali 117: Baadhi ya vijana wa nchii hii wanaenda katika miji mbalimbali na wanaona kwamba jambo hilo ni faradhi kwa kila mmoja baada ya kupewa fatwa na baadhi ya wanafunzi. Je, kitendo chao hichi ni sahihi?
Jibu: Haijuzu kwao kwenda isipokuwa kwa idhini ya mtawala. Kwa sababu wao ni raia na raia ni lazima kwake kumtii mtawala. Mtawala akiwapa idhini kutakuwa kumebaki vilevile radhi za wazazi wawili. Asisafiri isipokuwa kwa radhi ya baba yake. Kwa sababu alikuja mtu kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambapo akamuomba idhini ya kwenda Jihaad akamuuliza: “Je, wazazi wako wako hai?” Akajibu: “Ndio.” Akamwambia: “Kafanye Jihaad nao.” Baadaye akarudi kwa wazazi wake. Hiyo ni dalili inayofahamisha kwamba ni lazima kupatikane idhini ya wazazi wawili baada ya idhini ya mtawala.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa ´Ulamaa-ul-Kibaar fiy al-Irhaab wat-Tadmiyr, uk. 305
- Imechapishwa: 20/10/2019
Swali 117: Baadhi ya vijana wa nchii hii wanaenda katika miji mbalimbali na wanaona kwamba jambo hilo ni faradhi kwa kila mmoja baada ya kupewa fatwa na baadhi ya wanafunzi. Je, kitendo chao hichi ni sahihi?
Jibu: Haijuzu kwao kwenda isipokuwa kwa idhini ya mtawala. Kwa sababu wao ni raia na raia ni lazima kwake kumtii mtawala. Mtawala akiwapa idhini kutakuwa kumebaki vilevile radhi za wazazi wawili. Asisafiri isipokuwa kwa radhi ya baba yake. Kwa sababu alikuja mtu kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambapo akamuomba idhini ya kwenda Jihaad akamuuliza: “Je, wazazi wako wako hai?” Akajibu: “Ndio.” Akamwambia: “Kafanye Jihaad nao.” Baadaye akarudi kwa wazazi wake. Hiyo ni dalili inayofahamisha kwamba ni lazima kupatikane idhini ya wazazi wawili baada ya idhini ya mtawala.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa ´Ulamaa-ul-Kibaar fiy al-Irhaab wat-Tadmiyr, uk. 305
Imechapishwa: 20/10/2019
https://firqatunnajia.com/pata-idhini-kwa-mtawala-kisha-pata-radhi-za-wazazi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)