Swali: Kuna watu wanaosema kuwa kufunga siku moja pekee siku ya ´Aashuurah ndio Sunnah kwa sababu kitendo cha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kinatangulia kabla ya maneno yake. Je, mtazamo huu ni sahihi?
Jibu: Hapana, si sahihi. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mwishoni mwa uhai wake:
“Nikibaki mpaka mwaka ujao basi nitafunga tarehe tisa na kumi.”
Katika upokezi mwingine imekuja:
“… nitafunga siku kabla yake.”
Katika upokezi mwingine imekuja:
“… na siku baada yake.”
Lakini hii ina udhaifu ndani yake. Maneno yake:
“Nikibaki mpaka mwaka ujao basi nitafunga tarehe tisa na kumi.”
inapatikana katika “as-Swahiyh” ya Muslim. Maneno yanatangulia kabla ya kitendo. Maneno ndio msingi. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anaweza kusema jambo na huenda vilevile asilifanye kwa kutokuwa na uwezo. Anaweza kukokoteza kufunga, kama Dhul-Hijjah, na wala asiweze yeye kufunga kwa sababu ya kushughulika kwake na Da´wah, kueneza elimu, kuagiza majeshi na mengineyo. Sunnah inathibiti kwa maneno, vitendo na kulikubali jambo. ´Allaamah Ibn-ul-Qayyim amesema kuwa kuna njia tatu za kufunga:
Ya kwanza: Kufunga siku moja kabla yake na baada yake. Hili ndio bora zaidi. Huku ndani yake kuna kufunga siku tatu kwa mwezi.
Ya pili: Kufunga tarehe tisa na kumi.
Ya tatu: Kufunga tarehe kumi peke yake. Hili jambo ni sawa lakini hata hivyo limechukizwa. Mtu atakuwa ameafikiana na mayahudi katika jambo hili. Lakini hata hivyo halina neno.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (03) http://audio2.islamweb.net/lecturs/aalrrajhee/430/430.mp3
- Imechapishwa: 03/04/2018
Swali: Kuna watu wanaosema kuwa kufunga siku moja pekee siku ya ´Aashuurah ndio Sunnah kwa sababu kitendo cha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kinatangulia kabla ya maneno yake. Je, mtazamo huu ni sahihi?
Jibu: Hapana, si sahihi. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mwishoni mwa uhai wake:
“Nikibaki mpaka mwaka ujao basi nitafunga tarehe tisa na kumi.”
Katika upokezi mwingine imekuja:
“… nitafunga siku kabla yake.”
Katika upokezi mwingine imekuja:
“… na siku baada yake.”
Lakini hii ina udhaifu ndani yake. Maneno yake:
“Nikibaki mpaka mwaka ujao basi nitafunga tarehe tisa na kumi.”
inapatikana katika “as-Swahiyh” ya Muslim. Maneno yanatangulia kabla ya kitendo. Maneno ndio msingi. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anaweza kusema jambo na huenda vilevile asilifanye kwa kutokuwa na uwezo. Anaweza kukokoteza kufunga, kama Dhul-Hijjah, na wala asiweze yeye kufunga kwa sababu ya kushughulika kwake na Da´wah, kueneza elimu, kuagiza majeshi na mengineyo. Sunnah inathibiti kwa maneno, vitendo na kulikubali jambo. ´Allaamah Ibn-ul-Qayyim amesema kuwa kuna njia tatu za kufunga:
Ya kwanza: Kufunga siku moja kabla yake na baada yake. Hili ndio bora zaidi. Huku ndani yake kuna kufunga siku tatu kwa mwezi.
Ya pili: Kufunga tarehe tisa na kumi.
Ya tatu: Kufunga tarehe kumi peke yake. Hili jambo ni sawa lakini hata hivyo limechukizwa. Mtu atakuwa ameafikiana na mayahudi katika jambo hili. Lakini hata hivyo halina neno.
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (03) http://audio2.islamweb.net/lecturs/aalrrajhee/430/430.mp3
Imechapishwa: 03/04/2018
https://firqatunnajia.com/njia-tatu-za-kufunga-swawm-ya-aashuuraa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)