Swali: Sote tunatafuta kupata mwisho mwema katika dunia hii. Ni mambo yepi yanayosaidia muislamu kupata mwisho mwema?

Jibu: Kudumu juu ya matendo mema. Kwa sababu anayedumu juu ya jambo anahitimishwa nalo. Hivyo aendelee kudumu kufanya matendo mema na kumtii Allaah. Mtu kama huyu ana asilimia kubwa ya kumaliza vizuri. Vilevile mtu ajiepushe na mambo ya haramu na maasi ili asije kumaliza vibaya.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl (07) http://ajurry.com/safrawy/chorohat-elakida/charh-el-osol-el-thalatha/charh-fwzan/07.mp3
  • Imechapishwa: 25/01/2019