Swali: Ni lini mtoto anawajibika kufunga? Ni mpaka wa miaka mingapi ambayo anawajibika kufunga?
Jibu: Mtoto anaamrishwa kuswali anapofikisha miaka saba na anapigwa kwayo anapofikisha miaka kumi. Swalah hiyo itakuwa ni wajibu pindi atapobaleghe. Kubaleghe kunaptikana kwa moja ya mambo yafuatayo:
1- Kwa kutokwa na manii kwa matamanio.,
2- Kuota nywele sehemu za siri.
3- Kwa kuota usiku na akatokwa na manii.
4- Akafikisha miaka kumi na tano.
Mtoto wa kike anashirikiana na mtoto wa kiume katika mambo haya. Lakini yeye kuna kitu cha tano cha nyongeza alichonacho:
5- Hedhi.
Msingi wa hilo ni yale yaliyopokelewa na Imaam Ahmad na Abu Daawuud kutoka kwa ´Amr bin Shu´ayb, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa babu yake, aliyesimulia ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Waamrisheni watoto wenu swalah wanapokuwa na miaka saba, wapigeni kwayo wanapofikisha miaka kumi na watenganisheni katika vitanda.”
´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anh) amepokea vilevile ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kalamu imesimamishwa kwa watu aina tatu; kwa aliye lala mpaka aamke, mtoto mpaka abaleghe na kwa mwendawazimu mpaka awe na akili.”
Ameipokea Imaam Ahmad na amepokea mfano wa hiyo kutoka katika upokezi wa ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh). Ameipokea pia Abu Daawuud na at-Tirmidhiy ambaye amesema:
“Hadiyth ni nzuri.”
- Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (10/147-148)
- Imechapishwa: 31/05/2017
Swali: Ni lini mtoto anawajibika kufunga? Ni mpaka wa miaka mingapi ambayo anawajibika kufunga?
Jibu: Mtoto anaamrishwa kuswali anapofikisha miaka saba na anapigwa kwayo anapofikisha miaka kumi. Swalah hiyo itakuwa ni wajibu pindi atapobaleghe. Kubaleghe kunaptikana kwa moja ya mambo yafuatayo:
1- Kwa kutokwa na manii kwa matamanio.,
2- Kuota nywele sehemu za siri.
3- Kwa kuota usiku na akatokwa na manii.
4- Akafikisha miaka kumi na tano.
Mtoto wa kike anashirikiana na mtoto wa kiume katika mambo haya. Lakini yeye kuna kitu cha tano cha nyongeza alichonacho:
5- Hedhi.
Msingi wa hilo ni yale yaliyopokelewa na Imaam Ahmad na Abu Daawuud kutoka kwa ´Amr bin Shu´ayb, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa babu yake, aliyesimulia ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Waamrisheni watoto wenu swalah wanapokuwa na miaka saba, wapigeni kwayo wanapofikisha miaka kumi na watenganisheni katika vitanda.”
´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anh) amepokea vilevile ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kalamu imesimamishwa kwa watu aina tatu; kwa aliye lala mpaka aamke, mtoto mpaka abaleghe na kwa mwendawazimu mpaka awe na akili.”
Ameipokea Imaam Ahmad na amepokea mfano wa hiyo kutoka katika upokezi wa ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh). Ameipokea pia Abu Daawuud na at-Tirmidhiy ambaye amesema:
“Hadiyth ni nzuri.”
Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (10/147-148)
Imechapishwa: 31/05/2017
https://firqatunnajia.com/ni-lini-mtoto-anawajibika-kufunga-na-kuswali/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)