Swali: Sijui Hanafiyyah na Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) wanavojenga dalili pale wanaposema kuwa ni lazima kwa kila mmoja kuchinja Udhhiyah. Tukichukua maoni haya tukalinganisha ya yako pale uliposema kuwa kichinjwa cha msimamizi wa nyumba kinawatosha wakazi wa nyumba nzima, maoni ambayo yanaenda kinyume na maoni ya kwanza.

Jibu: Hawakusema kwamba kila mmoja achinje. Udhhiyah ni lazima kwa kiasi cha ilivyokuja katika Shari´ah. Hawakusema kuwa ni lazima kwa kila mmoja kuchinja. Ni lazima kwa wakazi wa nyumba wachinje. Lakini si lazima kila mmoja achinje. [… sauti haiko wazi…] Kitendo cha kila mmoja kuchinja kinaenda kinyume na Sunnah. Lakini midhali nyumba fulani ni wana uwezo basi haiwezekani wakaacha kuchinja.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://youtu.be/GYuXxoGgl2M
  • Imechapishwa: 06/07/2022